Mradi wa Majitaka Duga - Mwembeni
Imewekwa: 06 October, 2024
Mradi unathamani ya Shilingi Milioni 900 na unahusisha Ujenzi wa Mtandao wa Majitaka kutoka Duga hadi kituo cha kusukuma majitaka Makorora awamu ya tatu ambapo kazi kuu inayotekelezwa ni ulazaji wa mtandao wa mabomba ya majitaka kwa urefu wa km 3.2 na ujenzi wa kituo cha kusukuma majitaka eneo la Mikanjuni kwa lengo la kuboresha huduma hiyo na zaidi ya wananchi 500 katika kata za Duga, Msambweni na Makorora.

